Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 173 2024-02-13

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakarabati Jengo la OPD na kujenga uzio katika Kituo cha Afya Likombe - Mtwara Mikindani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Likombe ni moja ya vituo vya afya vilivyonufaika na mpango wa maboresho ambapo katika Mwaka wa Fedha 2017/2018, kituo hicho kilipokea shilingi milioni 500 na kujenga jengo la wazazi, maabara, jengo la kuhifadhia maiti, stoo ya dawa, nyumba ya mtumishi na kichomea taka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na maboresho makubwa yaliyofanywa katika kituo hicho, bado kuna uhitaji wa jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD) pamoja na uzio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara itatenga shilingi milioni 70 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje katika Kituo cha Afya cha Likombe. Ahsante. (Makofi)