Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 53 2023-11-03

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

Je, kwa nini Serikali isitumie teknolojia na vifaa vya kisasa kusafisha barabara za TANROADS?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imelichukua wazo la Mheshimiwa Mbunge na itaona ni namna gari nzuri ya kujumuisha teknolojia na vifaa vya kisasa katika kufanya usafi wa barabara pasipo kuathiri ajira za vikundi maalum ambavyo vimesajiliwa na Halmashauri za Miji, Wilaya, Mikoa, Manispaa na Majiji kwa kuzingatia matakwa ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2016, ahsante.