Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 178 2024-02-13

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza: -

Je, magari mangapi ya Zimamoto yanahitajika kukidhi mahitaji halisi nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Maurice Massaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linahitaji jumla ya magari 237 ya kuzima moto, magari 168 ya uokoaji, magari 28 ya HAZMAT, Crane 38, ambulance 168 na magari 28 ya ngazi ya kuzima moto katika majengo marefu (Turn table ladder). Serikali imeendelea kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kutenga fedha za maendeleo katika bajeti kila mwaka kwa ajili ya ununuzi wa magari ya kuzima moto pamoja na vifaa vingine vya uokoaji ambapo kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Jeshi limetengewa shilingi bilioni tatu kwa ajili ya ununuzi wa magari matano ya kuzima moto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ipo katika hatua za mwisho za kupata mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za Kimarekani milioni 100 utakaowezesha kupata vitendea kazi mbalimbali ikiwemo magari zaidi ya 100 ya kuzima moto na uokoaji kwa nchi nzima, ahsante.