Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 58 2023-11-03

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza:-

Je, nini Mkakati wa Serikali wa kuifanya Bandari ya Tanga iwe na ufanisi zaidi?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu sasa Bandari ya Tanga ilikuwa haihudumii meli na shehena ya kutosha kutokana na changamoto ya kasi ndogo ya huduma za meli na shehena hizo ambazo zilipaswa kuhudumiwa nangani umbali wa kilomita 1.7 kutoka gatini. Hali hii ilipunguza kwa kiasi kikubwa uwezo wa Bandari ya Tanga na ushindani wa bandari hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali kupitia TPA, inaendelea na maboresho ya bandari hiyo katika maeneo ya miundombinu, mitambo na vifaa ili kuvutia meli na shehena nyingi zaidi kama mkakati mahsusi wa kuifanya bandari hiyo ifanye kazi kwa ushindani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada hizo TPA ina mkakati mahsusi wa kimasoko kwa ajili ya Bandari ya Tanga ambao lengo lake ni kuteka soko la kaskazini mwa Tanzania na nchi jirani za Rwanda, Burundi, Uganda na DRC. Mikakati hiyo ni pamoja na kuwashawishi wateja wakubwa kutumia bandari hiyo kwa kutoa punguzo la tozo.