Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 71 2023-11-06

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO K.n.y. MHE. KASALALI E. MAGENI aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanzisha Halmashauri ya Wilaya ya Sumve ili kusogeza huduma kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kasalali Emmanuel Mageni, Mbunge wa Jimbo la Sumve, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kuanzisha maeneo mapya ya utawala upo kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa Sura ya 287 na 288 pamoja na Mwongozo wa Uanzishwaji wa Maeneo ya Utawala wa Mwaka 2014.

Mheshimiwa Spika, maombi ya kuanzisha Halmashauri mpya yanatakiwa kujadiliwa, kuridhiwa na kupitishwa kwenye vikao vya kisheria ngazi ya Vijiji, Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na Kamati ya Ushauri ya Mkoa kisha kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa tathmini ya vigezo.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kuboresha na kukamilisha miundombinu msingi kwenye maeneo ya kiutawala yaliyopo ili yaweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na baadaye kuendelea na maeneo mengine kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa, ahsante.