Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 74 2023-11-06

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:-

Je, kwa nini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Kijiji cha Mwagwila haukamiliki ingawa Serikali imetuma fedha nyingi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2013/2014 Serikali kupitia Mradi wa DASIP ilipeleka fedha za ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mwagwila yenye ukubwa wa hekta 250. Kazi iliyofanyika ni ujenzi wa banio na sehemu ya mfereji mkuu. Hata hivyo, kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha mradi huo haukuweza kukamilisha ujenzi wake.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha eneo lote linalofaa linamwagiliwa. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imetenga bajeti kwa ajili ya kufanya mapitio ya usanifu wa mradi huu ili kubaini gharama halisi ya kukamilisha ujenzi wa skimu hii. Aidha, ujenzi wa mradi huu utaanza mara baada ya kazi ya mapitio ya usanifu kukamilika.