Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 80 2023-11-06

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi mkubwa wa bilioni 41 wa kupeleka maji safi Ngara?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu,

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge Jimbo la Ngara Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maji inatarajia kutekeleza wa mradi mkubwa wa maji Ngara Mjini kwa gharama ya Shilingi bilioni 41. Usanifu wa mradi huu umekamilika na na unatarajiwa kuhudumia wananchi wapato 170,678 waishio katika Kata ya Ngara Mjini, Kanazi, Kibimba, Nyamiaga na Murukulazo. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha ili utekelezaji wa mradi huo uanze.

Mheshimiwa Spika, kwa mpango wa muda mfupi wa kupunguza kero ya maji katika Mji wa Ngara na viunga vyake, Serikali katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 imetenga kiasi cha fedha shilingi milioni 600. Kazi zitakazofanyika ni pamoja na uchimbaji wa visima viwili ambapo kisima kimoja kimekamilika, ujenzi wa tanki la ujazo wa lita 250,000 na ulazaji wa mtandao umbali wa kilometa 12 na ufungaji wa pampu mbili za kusukuma maji.