Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 81 2023-11-06

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kurejesha kwa wananchi eneo la Namajani - Masasi kwa vile Jeshi la Magereza limeshindwa kuwalipa fidia?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu,

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Ndanda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, baada ya kupokea malalamiko ya muda mrefu kutoka kwa wananchi Serikali iliwaelekeza wataalam wa ardhi wa Jeshi la Magereza na wataalam wa ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi kupima eneo lililovamiwa na kubaini kuwa na ukubwa wa ekari 2,054 na eneo ambalo halikuwa limevamiwa na wananchi lilikuwa na ekari 1,696.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Magereza kwa sasa linaendelea kumiliki eneo la ekari 1,696 ambazo hazikuwa na mgogoro. Kama hatua ya muafaka wa kumaliza mgogoro, Serikali ilikubali kuwaachia wananchi eneo lenye ukubwa wa ekari 2,054 lililokuwa tayari linatumiwa. Mwafaka huo ulifikiwa kwa kuwashirikisha wananchi wa Kijiji cha Ngalole, uongozi wa wilaya na Mkoa wa Mtwara, Wizara ya Ardhi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, nashukuru.