Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 85 2023-11-06

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza:-

Je, lini Serikali itakarabati viwanda vya kuchambua pamba vya Nyakarilo, Nyamirilo na Buyagu vilivyopo Sengerema?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, naomba kujibu la Mheshimiwa Hamis Mwagao Tabasam, Mbunge wa Jimbo la Sengerema, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, viwanda vya kuchambua pamba vilivyo na usajili wa Bodi ya Pamba hadi kufikia mwishoni mwa msimu 2022/2023 vilikuwa 92, na kati ya hivyo viwanda 57 vinamilikiwa na kampuni binafsi na 35 ni mali ya Vyama vya Ushirika.

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha viwanda vyote vya kuchambua pamba vinafanya kazi. Serikali kupitia Bodi ya Pamba (TCB) mwaka 2020 ilifanya tathmini ambayo imewezesha baadhi ya viwanda vinavyomilikiwa na vyama vya ushirika kupata mikopo kupitia Benki ya Kilimo iliyowezesha kukarabati viwanda vyao. Kupitia utaratibu huo, Serikali itahakikisha pia viwanda vya Nyakarilo, Nyamirilo na Buyagu vinakarabatiwa ili kuongeza tija katika mnyororo mzima wa sekta ya pamba. Nakushukuru.