Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 190 2024-02-13

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA Mkoa wa Songwe?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa sasa inatekeleza azma ya kujenga Chuo cha Ufundi katika kila Mkoa na Wilaya nchini. Katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali ilitenga shilingi bilioni 100 kwa ajili ya kujenga vyuo vya ufundi stadi katika Wilaya 64 ambazo zilikuwa hazijajengewa Vyuo vya Ufundi Stadi ikiwamo Chuo cha VETA cha Mkoa wa Songwe. Chuo cha VETA cha Mkoa wa Songwe kimetengewa fedha shilingi bilioni 6.53 kwa ajili ya ujenzi wa jumla ya majengo 25 ikijumuisha jengo la utawala, karakana, madarasa, maktaba, bwalo la chakula, vyoo, stoo pamoja na nyumba za watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshapeleka shilingi bilioni 1.14 kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA cha Mkoa wa Songwe ambapo kwa sasa ujenzi umefikia hatua ya kukamilika kwenye baadhi ya majengo na kazi ya ujenzi wa kuta inaendelea. Ahsante.