Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 140 2023-11-10

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: -

Je, lini Serikali itaweka mkakati maalum wa kumaliza mashtaka katika Bodi na Mahakama za Rufaa za Kodi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Janejelly Ntate, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Oktoba, 2023 Bodi ya Rufani za Kodi ilikuwa na mashauri 889 yenye kiasi cha kodi kinachobishaniwa cha shilingi trilioni 6.46 na dola za Kimarekani milioni 4.66. Katika kipindi hicho, Bodi imesikiliza mashauri 167 yenye kiasi cha kodi kinachobishaniwa cha shilingi trilioni 2.66 na dola za Kimarekani 200,001. Aidha, Baraza la Rufani za Kodi lilikuwa na mashauri 176 yenye kiasi cha kodi kinachobishaniwa cha shilingi bilioni 266.94, ambapo mashauri 91 yenye kiasi cha kodi kinachobishaniwa cha shilingi bilioni 166.32 yamesikilizwa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Bodi ya Rufani za Kodi na Baraza la Rufani za Kodi zinaendelea kutekeleza Mpango Maalum (Special Sessions) ambapo kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Juni, 2024 wanasikiliza na kumaliza mashauri ya kodi yaliyofunguliwa. Kupitia mpango huo, mashauri mengi zaidi yatasikilizwa katika Mikoa mbalimbali nchini kwa kuzingatia wingi wa mashauri haya ikiwemo Dar es Salaam, Arusha, Morogoro, Ruvuma, Tabora, Mara, Manyara, Kilimanjaro, Iringa, Mbeya, Songwe pamoja na Njombe.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia imeanzisha Taasisi ya Msuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi (Tax Ombudsman) ambayo jukumu lake kubwa itakuwa ni kupokea malalamiko na kutatua masuala ya kikodi yanayotokana na huduma, hatua za kikodi au utekelezaji wa sheria za kikodi kutoka kwa mlipakodi mbalimbali pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania.