Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 144 2023-11-10

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Mvomero ina jumla ya vijiji 129 ambapo kati ya hivyo, vijiji 92 tayari vimeshapatiwa umeme. Vijiji 37 vilivyosalia ambavyo baadhi vinapatikana katika Kata ya Kikeko, Kinda na Maskati vitapatiwa umeme na mkandarasi ambaye yupo maeneo ya mradi anaendelea na kazi za ujenzi wa miundombinu. Mkandarasi huyu anatarajia kukamilisha kazi ifikapo mwezi Juni, 2024, ahsante.