Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Madini 150 2023-11-10

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza: -

Je, lini Serikali itatoa leseni kwa wachimbaji wadogo wa madini Kata za Nditi na Kiegi – Nachingwea na maeneo mengine ya Mkoa wa Lindi?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amandus Julius Chinguile, Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini hadi Oktoba 2023, imetoa jumla ya leseni 2731 za uchimbaji mdogo wa madini katika Mkoa wa Lindi. Aidha, leseni zaidi ya 200 za Uchimbaji Mdogo wa Madini zimetolewa katika Vijiji vya Kiegei na Nditi Wilayani Nachingwea.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Madini itaendelea kutoa leseni za madini katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Wilaya ya Nachingwea na maeneo mengine ya Mkoa wa Lindi kadri itakavyokuwa ikipokea maombi ya leseni kutoka kwa wananchi ili kuwezesha ushiriki wao katika uchumi wa madini, ahsante sana.