Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 112 2024-02-07

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka alama za kuongoza meli katika eneo la kuegesha meli kwenye Ziwa Nyasa?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kama ifuatavyo:-

Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) ina mpango wa kujenga miundombinu ya bandari katika Ziwa Nyasa hususani Bandari ya Mbamba Bay. Ujenzi wa bandari hizi utahusisha pia usimikaji wa vifaa vya kuongozea meli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, TPA ina mpango wa kuweka alama za kuongozea meli katika bandari za maeneo mengine kuanzia mwezi Machi, 2024 kwani kupitia Mradi wa Upanuzi na Maboresho ya Miundombinu ya Bandari ya Dar es Salaam (Dar es Salaam Maritime Gateway Program – DMGP) maboya yaliyopo Bandari ya Dar es Salaam yataondoshwa kwa sababu mradi huo unahusisha pia uwekaji wa maboya mapya katika Bandari ya Dar es Salaam lakini kwa kuwa maboya hayo bado yapo katika matumizi yatasimikwa katika bandari nyingine.