Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 121 2024-02-07

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. JOSEPH A. TADAYO K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:-

Je, lini mradi wa maji wa Tukuyu utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Jimbo la Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na ukamilishaji wa Mradi wa Maji Tukuyu Mjini unaolenga kuhudumia wakazi wapatao 63,647 waishio kwenye Mitaa ya Mabonde, Kasyeto, Ndyonga, Batini, Bulyaga na Makandana. Utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa asilimia 85 ambapo kazi zilizotekelezwa hadi sasa ni pamoja na ujenzi wa banio katika chanzo cha Mto Mbaka, uchimbaji wa mtaro na ulazaji wa bomba kuu kutoka kwenye chanzo kwenda kwenye tenki umbali wa Kilometa 9.5, uchimbaji wa mtaro na ulazaji wa mabomba ya usambazaji, umbali wa kilometa 20 pamoja na ununuzi na ufungaji wa dira mpya za maji 125.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi zilizosalia ni ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji lenye uwezo wa lita 1,500,000 pamoja na ununuzi na ufungaji wa dira nyingine mpya 5,875 ambapo kazi zote hizi zinatarajiwa kukamilika mwezi Aprili, 2024.