Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 14 2023-11-01

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, Serikali haioni kigezo cha uzoefu katika kuomba kazi ni ubaguzi dhidi ya vijana waliohitimu vyuo wanaolenga kuingia katika soko la ajira?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, naomba kujibu swali lililoulizwa na Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ajira za Serikali zinatekelezwa kwa kuzingatia Sera ya Menejimenti na Ajira ya mwaka 2008. Kwa mujibu wa Aya ya 4.2(i) ya Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma inaelekeza kuwa Ajira kwa mara ya kwanza (entry point) hususan kwa wale wanaoajiriwa kwa cheo cha kuanzia kwenye miundo itafanyika kwa kuzingatia vigezo vya utaalam bila kujali uzoefu, isipokuwa kama kazi husika itahitaji kuwa na uzoefu.

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la uzoefu huwekwa kwenye nafasi ambazo si madaraja ya kuingilia kazini mfano nafasi za waandamizi, viongozi au kada ambayo uzoefu ndio sifa ya msingi ya kuingilia kama vile kada ya udereva ambapo lazima mtumishi huyu ajue kuendesha gari kwa viwango vilivyowekwa kwa mujibu wa Muundo wa Utumishi wa Kada hiyo.