Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 88 2023-11-07

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya kipaumbele katika Sekta ya Afya ni kupunguza vifo vya wajawazito, watoto chini ya miaka mitano na watoto wachanga kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ya msingi, katika kipindi cha mwaka 2015/2016 hadi kufikia 2022/2023 vifo vya wajawazito vimepungua kutoka vifo 556 katika kila vizazi hai 100,000 hadi 104 katika kila vizazi hai 100,000. Vifo vya watoto chini ya miaka mitano vimepungua kutoka vifo 67 katika kila vizazi hai 1000 hadi 43 katika kila vizazi hai 1000 mtawalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imetenga shilingi milioni 900 kwa ajili ya ukarabati wa hospitali Kongwe ya Mbozi. Pamoja na ukarabati na ujenzi wa miundombinu utakaofanyika katika hospitali ya Halmashauri ya Mbozi, kipaumbele kimewekwa kwenye jengo la huduma za mama na mtoto ikiwemo huduma za watoto njiti, ahsante.