Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 89 2023-11-07

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaboresha Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama kwa kujenga majengo ya upasuaji na wodi ili kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Kinyangiri na Mkalama vilivyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama ni miongoni mwa vituo vya Afya 199 chakavu ambavyo Ofisi ya Rais TAMISEMI imeviainisha kwa ajili ya kuvitafutia fedha na kuvifanyia ukarabati na upanuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ukarabati na kuongeza majengo kwenye vituo vya afya chakavu kote nchini vikiwemo vituo vya afya vya Kinyangiri na Mkalama. Vituo hivi vitapewa kipaumbele kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya upasuaji na wodi mara fedha zitakapopatikana, ahsante.