Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 105 2023-11-07

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na mrefu wa kukarabati Mradi wa Maji wa Makonde Mkoani Mtwara?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua Mradi wa Maji wa Makonde ni chakavu na unahitaji ukarabati. Katika mpango wa muda mfupi kwa mwaka 2023/2024, Serikali imetenga shilingi bilioni 1.5 ambapo tayari zaidi ya shilingi milioni 200 zimetolewa kwa ajili ya kufanya ukarabati wa mabomba ambapo, kazi ya ulazaji mabomba inaendelea na tayari umbali wa kilometa tano umekamilika kati ya 31 zilizopangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mpango wa muda mrefu, Serikali inaendelea na ukarabati mkubwa wa mradi wa Makonde kupitia mradi wa Maji wa Miji 28 utakaogharimu shilingi bilioni 84.7. Utekelezaji wa mradi huu umeanza mwezi Juni, 2022 na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024. Hadi sasa utekelezaji 40% umekamilika. Kwa mradi huu kutaondoa tatizo la maji katika Halmashauri ya Mji wa Newala, Wilaya ya Tandahimba na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba. (Makofi)