Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2023-11-08

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga chumba maalum yaani Incubator kwa ajili ya Mama na Watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya Ukerewe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe inatoa huduma kwa watoto wachanga na wale waliozaliwa kabla ya muda yaani Njiti. Hata hivyo, nafasi inayotumika kutolea huduma hiyo ni ndogo kwa mahitaji ya sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya inaendelea na uhakiki yaani assessment kwenye Hospitali zote za Halmashauri nchini ili kuweza kubaini mahitaji ya vyumba vya kuhudumia watoto njiti na kutafuta fedha kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa majengo hayo, ahsante.