Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 59 2024-02-02

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Je, lini Serikali italeta Bungeni sheria mahsusi kwa ajili ya kuwalinda wananchi dhidi ya ukatili wa kijinsia?

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Adamson Mwakasaka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunazo sheria zinazowalinda wananchi dhidi ya ukatili wa kijinsia ambazo ni Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16; Sheria ya Ndoa, Sura ya 29; Sheria ya Mtoto, Sura ya 13; Sheria ya Makosa ya Mtandao, Sura ya 443; na Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu, Sura ya 432. Kwa pamoja sheria hizo zina vifungu vinavyozuia makosa ya ukatili wa kijinsia. Sheria zote kwa pamoja zina vifungu vinavyoshugulika na makosa ya ukatili wa kijinsia. Hata hivyo, Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara nyingine za kisekta ikiwemo Wizara ya Maendeleo, Jinsia, Watoto na Makundi Maalum, Wizara ya Mambo ya Ndani, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania na wadau mbalimbali tunaendelea na uchambuzi ili kubaini iwapo ipo haja ya kuwa na sheria mahsusi ya ukatili wa kijinsia au tuboreshe sheria zilizopo. Baada ya kukamilika kwa uchambuzi huo Serikali itachukua hatua stahiki.