Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 4 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 112 2023-11-08

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kutoa motisha kwa watumishi wanaofanya kazi kwenye mazingira magumu?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Same Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutoa motisha za kifedha na zisizo za kifedha kwa watumishi wa Umma wakiwemo watumishi wanaofanya kazi katika mazingira magumu kwa kuboresha viwango vya posho za kazi baada ya masaa ya kazi, posho ya kujikimu wakati wa kusafiri, posho za mawasiliano, kufikisha huduma za umeme katika maeneo yao, kutoa magodoro na nyumba za walimu zenye staha na mengineyo mengi

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika Halmashauri yalipo maeneo yenye mazingira magumu kwa kutambua umuhimu wa kutoa motisha, zinatekeleza mipango yao ya motisha kwa kufuata miongozo inayotoka kwenye Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kusimamia utoaji wa motisha mbalimbali kwa watumishi hao kutegemeana na hali na mazingira magumu ya sehemu wanapofanyia kazi.