Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 8 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 133 2024-02-08

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: -

Je, ni lini jengo la huduma ya usafishaji damu kwa wagonjwa wa figo litajengwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Katavi?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Jimbo la Mpanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga shilingi bilioni tano kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi ambapo kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi 224,750,000 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la huduma ya usafishaji damu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)