Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 12 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 195 2024-02-14

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-

Je, lini Serikali itakamilisha mchakato wa kuanzisha Tarafa za Igoma na Mkolani – Nyamagana?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchakato wa kuanzisha Tarafa za Igoma na Mkolani, Nyamagana, ulijadiliwa na kuidhinishwa katika ngazi ya Kata, Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya na baadaye katika Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika tarehe 5 Novemba, 2018. Maombi hayo yaliwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa barua ya tarehe 18 Machi, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Serikali imetoa kipaumbele katika kuboresha na kukamilisha miundombinu kwenye maeneo ya kiutawala yaliyopo ili yaweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi na baadaye kuendelea na maeneo mengine kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa. Hivyo maombi ya kuanzisha Tarafa za Igoma na Mkolani katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza yatafanyiwa kazi na Serikali itakapoanza kuanzisha maeneo mapya ya utawala.