Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 1 East African Co-operation and International Affairs Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 16 2024-01-30

Name

Abdullah Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mahonda

Primary Question

MHE. ABDULLAH ALI MWINYI aliuliza:-

Je, nini maana ya non-aligned katika msimamo wa Tanzania Kimataifa wa kutofungamana?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdullah Ali Mwinyi, Mbunge wa Mahonda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, non-aligned ina maana ya kutofungamana ama kushikamana, kiitikadi na kimsimamo na nchi ama kundi la nchi zenye nguvu na ushawishi mkubwa duniani. Dhana hii ilikuja mara tu baada ya kumalizika kwa Vita Kuu ya Pili ya dunia mwaka 1945, ambapo dunia ilishuhudia kuibuka kwa kambi mbili zilizokuwa zinahasimiana ambazo ni Marekani na washirika wake chini ya mwamvuli wa NATO na uliokuwa Umoja wa Jamhuri za Kisoshalisti za Kisovieti (USSR) na washirika wake chini ya mwamvuli wa Warsaw Pact.

Mheshimiwa Spika, kufuatia hali hiyo, nchi ambazo ziliamini kutofungamana ama kuambatana na upande wowote zilianzisha Umoja wa Nchi Zisizofungamana na Upande Wowote (Non-Aligned Movement - NAM). Tanzania ilijiunga na umoja huu mwaka 1961 mara tu baada ya uhuru. Dhana ya kutofungamana na upande wowote ni miongoni mwa misingi ya sera yetu ya mambo ya nje.

Mheshimiwa Spika, kwa muktadha huo, Tanzania imeendelea kuwa mwanachama wa NAM kwa kutekeleza misingi ya kutofungamana na upande wowote katika maamuzi mbalimbali ambayo yanachukuliwa kwenye ajenda za kimataifa kwa kuzingatia uhuru na mipaka ya nchi (sovereignty and territorial integrity), kupinga matumizi ya nguvu za kijeshi, haki na usawa duniani na maslahi mapana ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.