Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 20 2024-01-30

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:-

Je, ni tafiti ngapi za mafuta zimefanyika nchini na yapi matokeo ya tafiti hizo?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, Kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania kwa kushirikiana na Kampuni za Kimataifa za Nishati imeendelea na tafiti za mafuta na gesi nchini kwa maeneo ya baharini na nchi kavu ambapo hadi kufikia mwezi Januari, 2024, jumla ya tafiti 84 zimefanyika.

Mheshimiwa Spika, kupitia tafiti ambazo zimeshafanyika, tumeweza kugundua uwepo wa gesi asilia tu. Hata hivyo, TPDC inaendelea na utafutaji wa mafuta katika maeneo ambayo yana viashiria vya uwepo wa mafuta. Maeneo hayo yanajumuisha bonde la Eyasi Wembere, Ziwa Tanganyika na bonde la Kilosa-Kilombero, ahsante.