Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 5 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 71 2024-02-05

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, biashara ya Kaboni katika misitu ya asili na ya kupanda imechangia kiasi gani kwenye pato la Taifa tangu iingie nchini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe Mkoani Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika miaka ya hivi karibuni kumeibuka soko huria la biashara ya kaboni ikijumuisha misitu ya asili na ya kupanda. Biashara hii ya kaboni imeanza kushamiri hapa nchini na kuonesha inaweza kuchangia kwenye pato la Taifa. Katika kipindi cha mwaka 2018 – 2022 fedha zilizopokelewa kupitia miradi inayotekelezwa kwenye halmashauri mbalimbali hapa nchini inafikia kiasi cha shilingi bilioni 32.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, hadi kufikia tarehe 31 Disemba, 2023 tumepokea jumla ya miradi mbalimbali 35 ya biashara ya kaboni, pindi mchakato wa usajili utakapokamilika na kuanza kutekelezwa kwa miradi hii, tunategemea kupata wastani wa dola za Marekani bilioni moja, sawa na shilingi trilioni 2.4 ambazo zitachangia kwa kiasi kikubwa kwenye pato la Taifa, ahsante.