Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 9 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 141 2024-02-09

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA aliuliza: -

Je, kuna mikakati gani kuhakikisha changamoto za Muungano ambazo hazijapatiwa ufumbuzi hazileti madhara nchini na lini zitapatiwa ufumbuzi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Zanzibar, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zimetengeneza utaratibu wa kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali za Muungano. Serikali za (SMT) na (SMZ) zimeunda Kamati ya pamoja ya (SMT) na (SMZ) ambayo huundwa na Wajumbe wa pande zote mbili za Muungano. Katika Kamati hii imesaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza changamoto nyingi za Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu kuanzishwa kwa Kamati ya Pamoja ya (SMT) na (SMZ) za Kushughulikia hizi kero za Muungano za mwaka 2006, hoja 25 zimepatiwa na kujadiliwa kwa lengo la kulipatia ufumbuzi. Kati ya hoja hizo, hoja 22 zimepatiwa ufumbuzi na kuondolewa kwenye orodha ya hoja ya changamoto za Muungano. Hoja zilizobakia zipo katika hatua mbalimbali za kuzipatia ufumbuzi na kwa kuwa Serikali zetu zote mbili za SMT na SMZ zina nia thabiti na dhahiri ya dhati ya kuhakikisha mambo yote yanayoletwa na changamoto katika utekelezaji wa masuala ya Muungano yanapatiwa ufumbuzi ni matumaini yangu ya kwamba hoja hizo zitapatiwa ufumbuzi hivi karibuni. Ahsante.