Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 212 2024-02-15

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kulipa fedha za madaraka kwa Waganga Wafawidhi wa vituo vya afya na zahanati nchini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kazi kubwa zinazofanywa na Waganga Wafawidhi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali za Halmashauri ambao ndio wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya katika ngazi ya msingi.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, iliaandaa andiko linaloonesha hitaji la kuwawezesha wasimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya kulipwa posho ya madaraka kama motisha kutokana na majukumu wanayotekeleza. Aidha, andiko hilo limewasilishwa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa hatua zaidi, ahsante.