Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 214 2024-02-15

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-

Je, kuna mkakati gani wa kujenga vituo vya afya kwenye kata za pembezoni mwa Mkoa wa Simiyu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha miaka mitatu ya fedha 2021/2022, 2022/2023 na 2023/2024 Serikali imejenga jumla ya vituo vya afya 466 vilivyogharimu shilingi bilioni 718.1 katika maeneo ya kimkakati kote nchini. Katika Mkoa wa Simiyu jumla ya vituo vya afya nane vimejengwa katika kata za kimkakati kwa gharama ya shilingi bilioni nne.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika kata za kimkakati kote nchini zikiwemo kata katika Halmashauri za Mkoa wa Simiyu.