Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 215 2024-02-15

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, nini kinakwamisha ujenzi wa barabara ya Same - Kisiwani - Ndungu hadi Mkomazi licha ya kutengewa fedha miaka minne mfululizo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya Same – Kisiwani – Ndungu hadi Mkomazi yenye urefu wa kilometa 98 ulikamilika mwezi Novemba, 2020 na uthamini wa mali za wananchi watakaoathirika na mradi ulikamilika mwezi Septemba, 2022. Baada ya kukamilika kwa kazi ya usanifu, Serikali ilianza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa kipande cha kilometa 5.2 kutoka Maore hadi Ndungu mwezi Septemba, 2021 ambapo kazi za ujenzi zinaendelea na zimefikia asilimia 55 na zinatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024.

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha taratibu za kusaini mkataba na makandarasi wawili ili kuanza kujenga sehemu iliyobaki yenye urefu wa kilometa 92.8 kwa kiwango cha lami ambayo imegawanywa katika sehemu mbili ambazo ni Same - Maore yenye urefu wa kilometa 56.8 na Ndungu - Mkomazi yenye urefu wa kilometa 36, ahsante.