Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 217 2024-02-15

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS aliuliza: -

Je, lini Serikali itaajiri Maafisa Mifugo katika kila Kata ili kuwasaidia wafugaji?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Venant Daud Protas, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mwongozo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa utoaji huduma za ugani wa mwaka 2011 unaelekeza katika kila Kata na kila Kijiji kuwa na Afisa Ugani. Hata hivyo, idadi ya Maafisa Ugani wa Mifugo waliopo kwa sasa ni 4,406 ikilinganishwa na mahitaji ya Wagani 20,537 nchini, sawa na upungufu wa Maafisa Ugani 16,131.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na upungufu uliopo na kuongeza wigo wa utoaji huduma za ugani, Serikali imeendelea kuajiri Maafisa Ugani kila mwaka, ambapo kati ya mwaka 2021 hadi 2023 jumla ya Maafisa Ugani 1,205 waliajiriwa na kupangiwa vituo katika Kata na Vijiji mbalimbali hapa nchini. Aidha, Wizara inaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais - TAMISEMI kuomba vibali zaidi vya ajira za Maafisa Ugani na kuendelea kuajiri Maafisa Ugani kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.