Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 13 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 219 2024-02-15

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Serikali kuongeza uzalishaji wa zao la pareto?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Rose Cyprian Tweve, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali ya kuongeza uzalishaji wa zao la pareto. Mikakati hiyo ni pamoja na kuimarisha utafiti wa zao hilo ili kubadili kilimo kuwa cha kibiashara, chenye tija, himilivu na kushirikisha sekta binafsi ili kuwa na kilimo endelevu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia misingi hiyo ya kuleta mageuzi katika kilimo cha zao la pareto, katika mwaka 2021/2022 Serikali ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 200 kwenda Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) kwa ajili ya kuzalisha mbegu bora za pareto ambapo kiasi cha kilo 1,400 zimezalishwa na kusambazwa kwa wakulima katika msimu wa mwaka 2023/2024. Mbegu hizo zinatarajiwa kupandwa katika eneo la ekari 5,600 na kuzalisha wastani wa tani 2,240 za maua ya pareto.