Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Finance and Planning Wizara ya Fedha 128 2024-04-19

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-

Je, lini Serikali italipa fidia eneo la Makaburi Idefu – Makambako ili kupisha ujenzi wa One Stop Centre?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshalipa fidia ya shilingi bilioni 4.6 kwa wananchi waliopisha eneo kwa ajili ya Mradi wa Ujenzi wa One Stop Centre. Aidha, Serikali imeanza taratibu za tathmini ya eneo la makaburi ya Idefu, Makambako na taratibu za malipo zitaanza baada ya kuidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali.