Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 130 2024-04-19

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MIRAJI J. MTATURU aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Ikungi – Mang'onyi – Londoni hadi Kilimatinde?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, zabuni ya manunuzi kwa ajili ya kumpata mhandisi mshauri wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa Barabara ya kutoka Ikungi – Mang’onyi – Londoni hadi Kilimatinde yenye urefu wa kilometa 117.8 iko katika hatua za mwisho. Mkataba wa kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina utakuwa umesainiwa kabla ya mwezi Juni, 2024. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina inatarajiwa kuchukua kipindi cha mwaka mmoja na nusu, hivyo zitakamilika mwezi Disemba, 2025.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)