Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 377 2024-05-20

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa njia ya umeme ya msongo mkuu Tabora – Mpanda utakamilika?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia TANESCO inatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kilovoti 132 yenye urefu wa kilometa 383 kutoka Tabora hadi Mpanda, Katavi lengo likiwa ni kuunganisha Mkoa wa Katavi katika Gridi ya Taifa. Gharama za mradi huu ni shilingi bilioni 116. Aidha, utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Septemba, 2022 na umefikia 58%, ahsante.