Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 379 2024-05-20

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Madaraja ya Bujonde na Ilondo Mwaya - Kyela utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ujenzi wa Daraja la Bujonde linalounganisha Kata ya Kajunjumele na Bujonde. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina imefikia 85% na inatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni, 2024. Baada ya kazi ya usanifu kukamilika, Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Daraja la Ilondo - Mwaya, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikiwa ni maandalizi ya kulijenga daraja hili, ahsante.