Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 29 Finance Wizara ya Fedha 386 2024-05-20

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE K.n.y. MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je, ni nini msingi kwa wafanyabiashara kutoza bei tofauti au fedha za kigeni kwa wateja ambao ni raia wa kigeni na nini athari zake?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, Serikali imeandaa sheria na kanuni ili kumlinda mlaji na kuhakikisha kuwa bei za bidhaa na huduma zinapangwa kwa msingi wa nguvu ya soko. Kwa mantiki hii, biashara zimekuwa zikiendeshwa chini ya utaratibu wa soko huria ambapo bei za bidhaa na huduma hupangwa kuendana na uwiano wa uhitaji na upatikanaji wa bidhaa husika. Hata hivyo, wafanyabiashara wanaweza kutoza bei tofauti kwa bidhaa na huduma baina ya wazawa na raia wa kigeni au kwa fedha za kigeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande mwingine Serikali inatambua na imeendelea kukumbusha kuwa shilingi ndio fedha halali kwa ajili ya malipo mbalimbali hapa nchini. Kutokana na hilo, raia wa kigeni hawatakiwi kulazimishwa kulipa kwa fedha za kigeni hususan pale wanapokuwa na shilingi za Kitanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, wageni wanaruhusiwa kutumia fedha za kigeni ili kurahisisha ufanyaji wa biashara pale wanapokosa shilingi za Kitanzania na viwango vya ubadilishaji fedha havikitakiwi kutofautiana na vile vinavyotozwa katika masoko ya fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna athari za kimsingi za uchumi kwa wafanyabiashara kutoza bei tofauti baina ya wateja raia wa kigeni na wazawa kwani bei hizo huamuliwa katika soko huru na hivyo inatarajiwa kupanda na kushuka kulingana na nguvu za mahitaji na ugavi sokoni, ahsante. (Makofi)