Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 52 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 456 2022-06-27

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FATMA H. TOUFIQ K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa treni ya mwendokasi kutoka Kaliua-Mpanda hadi Karema?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TRC imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali wa ujenzi wa njia ya reli ya Kaliua – Mpanda – Karema kwa kiwango cha Standard Gauge. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi wa reli hii.