Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 43 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 559 2024-06-07

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwawezesha wadau wa michezo kuwekeza katika kuzalisha vipaji vya michezo mbalimbali hasa mpira wa miguu?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inayo mikakati mbalimbali ya kuwawezesha wadau wake kuwekeza katika kuzalisha vipaji vya michezo hususan mpira wa miguu ikiwemo kuandaa miongozo na kanuni mahususi zinazowalinda wadau wanaoanzisha shule maalumu za kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo (sports academies) ili kuhakikisha wananufaishwa na uwekezaji wanaoufanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hatua kadhaa nyingine, Serikali inawaunganisha wadau hao na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania kupitia programu kadhaa za kuibua na kuendeleza vipaji zikiwemo UMITASHUMTA, UMISETA na UMISAVUTA. Aidha, Serikali imeanzisha mafunzo ya elimu ya michezo ngazi za Astashahada na Stashahada katika vyuo sita nchini vikiwemo Vyuo vya Ualimu Butimba, Korogwe, Mpwapwa, Monduli na Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya. Hali kadhalika, Serikali inaendelea kuimarisha utoaji wa mafunzo ya shahada ya kwanza katika elimu ya michezo kwenye Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa lengo la kuongeza idadi ya wataalamu wa kufundisha michezo ili kupunguza gharama za uwekezaji.