Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 41 Investment and Empowerment Ofisi ya Rais TAMISEMI. 344 2016-06-13

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-
Katika Ilani ya CCM 2016/2017 Serikali imeahidi kuinua kipato cha mwananchi mmoja mmoja:-
Je, ni lini Serikali itaanza kutoa fedha kiasi cha shilingi 50,000,000 kwa kila Kijiji au Mtaa ili kuwasaidia wananchi kuboresha mitaji yao?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetenga shilingi bilioni 59.5 katika bajeti ya mwaka 2016/2017 chini ya Fungu 21, kwa ajili ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 ya kupeleka shilingi milioni 50 kwa kila kijiji. Fedha hizo zitatolewa baada ya kukamilisha taratibu mahususi zinazolenga kuhakikisha uwepo wa tija, katika matumizi ya fedha hiyo. Hivyo namwomba Mheshimiwa Mbunge Jacqueline, asubiri utekelezaji wake kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017. Mara baada ya kukamilika kwa mfumo na muundo wa utekelezaji wa zoezi zima, ambapo kazi hii imeshaanza kufanyika.