Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 197 2024-04-29

Name

Janeth Maurice Massaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y. MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa dharura wa kujenga barabara kwa kiwango cha lami pembezoni mwa reli ya SGR wakati ujenzi unaendelea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Reli Na. 10 ya mwaka 2017, hifadhi ya reli ni meta 30 kutoka katikati ya reli kila upande. Katika eneo hili hairuhusiwi kujenga barabara kwa matumizi ya kawaida. Hivyo, haitawezekana kujenga barabara ya lami pembezoni mwa reli ya SGR, ahsante. (Makofi)