Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 15 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 200 2024-04-29

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Mahakama mpya katika Kata za Chala na Kate Jimbo la Nkasi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Nkasi Kusini, kama ifuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania inaendelea kuboresha miundombinu ya majengo ya Mahakama hususan kwa ngazi ya Mahakama za Mwanzo ambako ndiko kwenye changamoto kubwa ya uhaba na uchakavu wa majengo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kata za Kate na Chala wanapata huduma za Mahakama ndani ya kata zao katika Mahakama ya Kate na Chala japo majengo ya Mahakama hizi ni chakavu. Kulingana na mpango wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama, katika mwaka wa fedha 2023/2024 tunajenga Mahakama ya Mwanzo Namanyere na katika mwaka wa fedha 2024/2025 tutajenga Mahakama ya Mwanzo Kate.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele cha Mahakama ni kujenga majengo ya Mahakama za Mwanzo katika maeneo ambayo hakuna kabisa huduma za Mahakama ili kuwapunguzia wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za kimahakama. Ahsante sana.