Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu: Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu | 51 | 2025-01-31 |
Name
Tecla Mohamedi Ungele
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka huduma za Mifuko ya Jamii ngazi ya Wilaya na Tarafa ili kuwaondolea usumbufu Wastaafu kwenda kuhakikiwa Mkoani?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, naomba kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, kwa sasa uhakiki wa uanachama unafanyika katika Ofisi za Mifuko zilizopo mikoani na wilayani. Pili, Mifuko imefanya maboresho zaidi katika matumizi ya TEHAMA ambapo kwa sasa mstaafu anaweza kujihakiki mwenyewe kupitia simu janja (smartphone) kwa kutumia programu ya kidijitali (Online Portal) bila kuhitaji kufika katika Ofisi za Mifuko.
Mheshimiwa Spika, kwa maelezo hayo, ukusanyaji wa taarifa ni shirikishi toka ngazi zote zikiwemo ngazi za tarafa, wilaya hadi mkoani, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved