Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 4 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 52 | 2025-01-31 |
Name
Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vwawa
Primary Question
MHE. JAPHET N. HASUNGA aliuliza: -
Je, ni lini TARURA itaanza ujenzi wa barabara ya Vwawa- Iganduka hadi Isalalo kwa kiwango cha lami?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, barabara ya Vwawa - Iganduka hadi Isalalo ipo kwenye mpango wa uboreshaji wa miji na majiji chini ya Program ya TACTIC inayofadhiliwa na Benki ya Dunia katika kundi la tatu (Tier III), ambapo kwa awamu ya kwanza barabara yenye urefu wa kilomita 2.0 itajengwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Spika, kuanzia Januari, 2025, wataalam wa usanifu wameanza kuripoti katika miji 18 ya kundi la tatu ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Vwawa kuanza kazi ya usanifu kwa kipindi cha miezi sita. Baada ya usanifu kukamilika tunatarajia kutangaza zabuni za kuwapata Wakandarasi na washauri elekezi kupitia mfumo wa NeST ifikapo Juni, 2025 na taratibu za ununuzi zitakamilika Oktoba, 2025 ili Wakandarasi watakaopatikana waanze utekelezaji mara moja ndani ya mwezi huo wa Oktoba, 2025.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara za lami katika Makao Makuu ya Miji ya Wilaya ikiwemo Vwawa, Songwe kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved