Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 8 | 2025-01-28 |
Name
Maida Hamad Abdallah
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA K.n.y. MHE. MAIDA HAMADI ABDALLAH aliuliza:-
Je, lini Serikali itawalipa madai ya muda mrefu Askari Polisi waliomaliza muda wao?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kulipa madai ya askari Polisi waliomaliza muda wao wa kazi baada ya kustaafu, jumla ya fedha kiasi cha shilingi 97,120,011,700.26 zinadaiwa. Mpaka sasa madai yaliyohakikiwa na kuwasilishwa Wizara ya Fedha kwa ajili ya malipo ni shilingi 75,214,744,005.10. Kwa sasa madai yanayoendelea kuhakikiwa ni ya Mwaka wa Fedha 2023/2024 na kiasi cha fedha shilingi 21,905,267,695.16 zinadaiwa.
Mheshimiwa Spika, pindi uhakiki ukikamilika madai yote yatawasilishwa Wizara ya Fedha kwa ajili ya malipo. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved