Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 9 | 2025-01-28 |
Name
Iddi Kassim Iddi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Msalala
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Makao Makuu ya Polisi katika Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala ina kituo cha polisi daraja B ambacho kinakidhi mahitaji ya kutoa huduma ya polisi kwa wananchi wa Msalala. Kituo hiki kipo eneo la Bugarama na kina miundombinu yote ya msingi ikiwemo Ofisi za Mkuu wa Polisi wa Wilaya (OCD), Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai wa Wilaya (OC-CID), Mkuu wa Kituo (OCS), Ofisi ya Makosa ya Usalama Barabarani pamoja na Ofisi ya Dawati la Kushughulikia Ukatili wa Kijinsia. Kituo hiki kitatumika kama Makao Makuu ya Polisi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kahama. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved