Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 18 Sitting 1 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 15 2025-01-28

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: -

Je, lini Halmashauri ya Wilaya ya Maswa itapewa CSR inayotokana na uwepo wa Mradi wa SGR?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, mikataba ya ujenzi inayoingiwa kati ya TRC na mkandarasi imeendelea kuzingatia suala la uwajibikaji kwa jamii yaani Corporate Social Responsibility (CSR) kwa kutenga fedha. Aidha, Mradi wa Ujenzi wa Reli ya SGR umeendelea kutoa CSR katika maeneo ambapo mradi unapita na mpaka sasa mradi umefadhili miradi mbalimbali yenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 9.5. Kwa upande wa Wilaya ya Maswa, kwa kuanzia Mradi wa Ujenzi wa Reli ya SGR kwa kipande cha Isaka-Mwanza umeshatoa CSR yenye thamani ya shilingi milioni 28.4 ambazo kwa kuanzia zimeelekezwa kwenye mradi wa bweni la wanafunzi katika shule ya Sekondari ya Wasichana Mataba, Mwasalage na ujenzi wa Shule ya Sekondari Mashimba.