Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 15 | 2025-01-28 |
Name
Mashimba Mashauri Ndaki
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Maswa Magharibi
Primary Question
MHE. MASHIMBA M. NDAKI aliuliza: -
Je, lini Halmashauri ya Wilaya ya Maswa itapewa CSR inayotokana na uwepo wa Mradi wa SGR?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, mikataba ya ujenzi inayoingiwa kati ya TRC na mkandarasi imeendelea kuzingatia suala la uwajibikaji kwa jamii yaani Corporate Social Responsibility (CSR) kwa kutenga fedha. Aidha, Mradi wa Ujenzi wa Reli ya SGR umeendelea kutoa CSR katika maeneo ambapo mradi unapita na mpaka sasa mradi umefadhili miradi mbalimbali yenye thamani zaidi ya shilingi bilioni 9.5. Kwa upande wa Wilaya ya Maswa, kwa kuanzia Mradi wa Ujenzi wa Reli ya SGR kwa kipande cha Isaka-Mwanza umeshatoa CSR yenye thamani ya shilingi milioni 28.4 ambazo kwa kuanzia zimeelekezwa kwenye mradi wa bweni la wanafunzi katika shule ya Sekondari ya Wasichana Mataba, Mwasalage na ujenzi wa Shule ya Sekondari Mashimba.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved