Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 1 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 16 | 2025-01-28 |
Name
Bakar Hamad Bakar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
House of Representatives
Primary Question
MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN K.n.y. MHE. BAKAR HAMAD BAKAR aliuliza:-
Je, ni kiasi gani Serikali inahakikisha vyombo vya usafiri majini vinatimiza takwa la kuwa na vifaa vya uokozi kwa abiria?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TASAC inachukua hatua mbalimbali katika kuhakikisha vyombo vya usafiri majini vinatimiza takwa la kuwa na vifaa vya uokozi kwa abiria. Hatua hizo ni kama ifuatavyo:-
(i) Ukaguzi wa vyombo vyote vya usafiri majini na utoaji wa vyeti vya ubora. Ukaguzi huu unahakikisha vyombo vina vifaa vya uokozi kama maboya ya kujiokoa kwa abiria wote;
(ii) Kutoa elimu kwa jamii na kampeni maalum kwa jamii zinazoishi maeneo yanayozungukwa na maji. Lengo ni kuwafundisha wamiliki wa vyombo na abiria umuhimu wa vifaa vya uokozi na taratibu za usalama; na
(iii) Kampeni za usalama wakati wa sikukuu ili kuhakikisha havizidishi idadi ya abiria iliyoainishwa kwenye vyeti vyao. Vyombo vinavyoshindwa kufuata sheria hupigwa faini hadi shilingi milioni 6.25 kwa vyombo vikubwa (zaidi ya mita 24) na shilingi laki nne kwa vyombo vidogo (chini ya mita 24).
Mheshimiwa Spika, vilevile Tanzania kupitia TASAC inatekeleza mikataba ya Shirika la Bahari Duniani yaani International Maritime Organization (IMO) kama SOLAS (Safety of Life at Sea Convention). Mkataba huo wa lazima kwa nchi mwanachama pamoja na mambo mengine unalazimisha vyombo vya usafiri majini kuwa na vifaa vya uokozi ambavyo vinakidhi viwango vya kimataifa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved