Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 18 | Sitting 6 | Information, Culture, Arts and Sports | Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo | 105 | 2025-02-04 |
Name
Asha Abdullah Juma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kuinua lugha ya Kiswahili kupitia vyombo vyake vya habari vya kitaifa?
Name
Hamis Mohamed Mwinjuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muheza
Answer
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) inatekeleza mikakati mbalimbali ya kuinua na kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili kupitia vyombo vya habari vya kitaifa kama vile redio, televisheni, makala za magazeti na mitandao ya kijamii. Serikali imeweka msisitizo kwa vyombo vya habari vya kitaifa, kuandaa na kurusha vipindi vinavyoelimisha, kuburudisha na kuhamasisha matumizi ya Kiswahili fasaha.
Mheshimiwa Naibu Spika, vipindi hivi vinahusisha mijadala ya kitaaluma, tamthilia, mashairi, na makala zinazochambua masuala ya lugha na utamaduni. Kwa sasa idadi ya vipindi imeongezeka hadi kufikia 35 kwa wiki.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved